October 31, 2009

SIMBA KIDEDEA


Simba SC yairarua Dar Young African watoto wa jangwani kwa bao moja bila lililofungwa kimyani na Musa Mgosi na hivyo kuweka rekodi yakutopoteza mechi hata moja katika mzunguko wa kwanza.

Jahazi yazindua daktari wa mapenzi








mashabiki wakiramba arambaa arambaaaa.....




Jahazi modern taarab chini ya bingwa wa mapenzi Mzee Yusuf imezindua albamu ya tano inayokwenda kwa jina la DAKTARI WA MAPENZI katika ukumbi wa diamond Jubilee. Hakika mapenzi yalipata daktari kwani mashabiki walikongwa roho zao kisawasawa......

October 27, 2009

wafungaji bora duniani

ANTONIO DI NATALE UDINESE 9 SERIE A
ANDERSON NENE MONACO 9 LIGUE 1
JOHN BOKO AZAM FC 8 VODACOM Tanzani
DIDIER DROGBA CHELSEA 8 PREMIER LEAGUE
FERNANDO TORRES LIVERPOOL 8 PREMIER LEAGUE
HUSSEIN BUNU JKT RUVU 7 VODACOM Tanzania
WAYNE ROONEY MAN UTD 6 PREMIER LEAGUE
CRISTIANO RONALDO REAL MADRID 5 LA LIGA

October 25, 2009

raha ya koko bichi

Koko bichi ni moja ya fukwe maarufu kwa wakazi wengi wa jijini Dar kwa wananchi wengi kwenda kupumzika na kubadilishana mambo mawili matatu. Hapa pamekuwa ni moja ya maeneo maarufu kwa upatikanaji wa mix, mishikaki, mihogo n.k

October 24, 2009

SIMBA 1 AZAM 0

Simba SC yadhihilisha ubabe wake kwa Azam FC kwa kuichapa bao moja bila katika uwanja wa uhuru jijini Dar es Salaam

in reference to: Google (view on Google Sidewiki)

October 23, 2009

simba zaidi ya Manchester united



Simba sports club imeonyesha kuwa iko juu zaidi ya manchester united ya nchini uingereza kwa kuweza kufikisha point 24 ikiwa imecheza mechi 8 bila ya kupoteza mechi hata moja huku manchester wakiwa na point 22 na mchezo mmoja mbele ya simba. Wakati simba inakutana tarehe 31 oct na watani wao Yanga, manchester nao watakuwa na kazi ngumu ya kukutana na Liverpool jumapili ya tarehe 24 oct. Nani kati yao ataibuka mshindi?

October 19, 2009

Nafasi kwa mtoto



katika maisha ya sasa haya tuliyonayo mtoto anahitaji sana nafasi ya kuweza kujifunza mambo mbalimbali na hapo ndipo utakapoweza kutambua kipaji alichonacho kama mzazi juu ya mtoto wako. Hili bado halijawa jambo rahisi kwetu watanzania tukidhani kuwa hayo ni kwa wenzetu wazungu. Ninachoweza sema juu ya hili ni kwamba kila mzazi anayohaki yakumpatia mtoto wake malezi yaliyo bora ili mradi tu hayaendi kinyume na maadili ya malezi kwa mtoto.

Fukwe zetu









Hakika fukwe zetu zinamuonekano mzuri na wakuvutia.

October 14, 2009

Mwanza yaweka rekodi


Kwa mara nyingine tena Jiji la Mwanza laweka historia nyingine baada ya kijana Pascal Cassian kujinyakulia taji la BSS 3 na kujipatia kitita cha Tsh 25mil na kuwaangusha vinara wawili Peter Msechu kutoka Kigoma na Kelvin Mbati kutoka jiji la Lukuvi Dar Es Salaam. Ikumbukwe pia Miss Tanzania 2009 anatokea huko.

October 13, 2009

miaka 10 bila ya Mwl. J. K. Nyerere



Ni miaka kumi tangu mwl. J. K. Nyerere mwanzilishi wa taifa letu kututoka. Ni siku ya tarehe 14.10.1999 ndipo taifa lilipotwa na mshituko wa aliyekuwa baba wa taifa letu kipenzi cha watu kuwa ameaga dunia. Maswali mengi yalikuja vichwani mwa walio wengi juu ya namna taifa letu changa litakavyokuwa bila yeye. Japo mambo mengi aliyoyatabiri kuwa yatatokea kama yasiposhughulikiwa ndio yamejitokeza mfano ulimbikiziaji wa mali na mgongano wa kisiasa wa Zanzibar na mengine mengi. Imekuwa ni jadi yetu kama taifa kumkumbuka kila ifikapo tarehe 14. Je yale aliyoyaacha yanafuatwa? Viongozi wanakumbuka miiko ya uongozi? Mungu ilaze mahali pema roho yake amen.

Pregnant Woman Pregnant Again, Julia Grovenburg Conceives Consecutively - ABC News

facebook
Stephen Bendera
9:45am Oct 13th
Pregnant Woman Pregnant Again, Julia Grovenburg Conceives Consecutively - ABC News
To stezuvehra.1977@blogger.com
 
pregnant woman pregnant again

Stephen has shared a link to a news story with you. To view the news story or to reply to the message, follow this link:

http://www.facebook.com/p.php?i=1085725357&k=Z6MY53RXPYTF6BD1QAWXYUWQ2RIB4XZ1QWCPA&oid=1064566433891
If you do not wish to receive this type of email from Facebook in the future, please click here to unsubscribe.
Facebook's offices are located at 1601 S. California Ave., Palo Alto, CA 94304.

October 12, 2009

Hepi bethidei Paul Amani Bendera




Familia ya bwana na bibi Edward Paul Amani wa Lugalo wanayofuraha ya kumpongeza mtoto wao kipenzi Paul kwa kutimiza mwaka mmoja. Tunakutakia afya njema na makuzi mema.

October 09, 2009

Nobel Peace Price


Rais Barack Obama wa marekani ametunukiwa tuzo ya amani ya Noble Peace Price 2009 ikiwa ni muda mfupi tu tangu kuingia kwake madarakani.

October 08, 2009

Afya ya JK iko bomba


Madaktari wa rais J.K wathibitisha kuwa rais yuko fit katika kulitumikia Taifa letu la Tanzania.

October 07, 2009

Rais Jakaya Kikwete atimiza miaka 59


Tunakutakia birthday njema na afya tele katika kuliendesha taifa letu la Tanzania kwa amani na mshikamano.

October 05, 2009

mgao wa umeme



Mgao wa umeme ulionza hivi karibuni wawa chanzo cha kuzorota kwa kipato kwa wananchi hasa wakipato cha chini kutokana na shughuli za uendeshaji uchumi kusimama. Misongamano ya magari nayo yawa kero kwa watumiaji wa magari jijini. 

October 04, 2009

usiku wa maraha




Hapa Babu njenje akiimba wimbo wa kisebu sebu unaopendwa sana na wadau wa njenje

Nyota Waziri akiimba wimbo wa gere na staili ya kijoti joti hakika hapatoshi



anko Kitime akicharaza gita

Kwa raha kamili kutana uso kwa uso selender bridge kila siku ya Jumamosi

October 03, 2009

MIRIAM GERALD NDIYE VODACOM MISS TANZANIA 09


Baada ya kusubiriwa kwa muda mrefu hatimaye Miriam Gerald toka kanda ya ziwa atwaa taji la vodaacom miss Tanzania 2009 na kujinyakulia gari aina ya Grand vitara na pesa taslimu mil 9.

October 02, 2009

HOMA YAZIDI KUPANDA MISS TANZANIA

Homa yazidi kuwapanda warembo wanoawania taji la Vodacom miss Tanzania litakalofanyika mapema leo hii katika ukumbi wa kisasa wa mlimani city, jijini Dar Es Salaam. Mshindi kujinyakulia gari aina ya suzuki Grand lenye thamani ya sh mil. 53.2 na fedha taslimu sh mil 9.

NANI KUCHEKA KASEBA AU FRANCIS CHEKA?

LEO NDIO LEO SIKU ILIYOKUWA IKISUBIRIWA NA WADAU WENGI WAPENDAO MCHEZO WA NGUMI NCHINI KATI YA BINGWA WA MABARA WA KICKBOXING JAPHET KASEBA NA FRANCIS CHEKA ANAYESHIKILIA UBINGWA WA DUNIA WA ICB. MPAMBANO HUO UTAKAOKUWA WA RAUNDI 12 UTAFANYIKA KATIKA UWANJA WA UHURU JIJINI DAR ES SALAAM.